sw_tw/bible/other/fellowshipoffering.md

611 B

sadaka ya ushirika

Ufafanuzi

Katika Agano la Kale, "sadaka ya ushirika" ilikuwa aina ya sadaka ambayo ilitolewa kwa sababu tofauti, kama vile kutoa shukrani kwa Mungu na kutimiza kiapo.

Sadaka hii ilihitaji sadaka ya mnyama, ambaye alikuwa wa kiume au kike. Hii ilikuwa tofauti na sadaka ya kuteketeza ambayo ilihitaji mnyama wa jinsia ya kiume.

Baada ya kutoa sehemu ya sadaka kwa Mungu, mtu aliyeleta sadaka ya ushirika aligawana nyama na makuhani na Waisraeli wengine.

Kulikuwa na mlo unaohusishwa na sadaka hii ambayo hujumuisha mkate usiotiwa chachu.

Hii mara zingine unaitwa "sadaka ya amani"