sw_tw/bible/other/father.md

1.3 KiB

mhenga, baba, mababu

Ufafanuzi

Inapotumika kihalisia, msemo "baba" una maana ya mzazi wa kiume wa mtu. Kuna baadhi ya matumizi ya tamathali ya msemo huu.

Misemo "baba" na "babu" hutumika kumaanisha mababu wa mtu fulani au kundi la watu. Hii inaweza kutafsiriwa kama "babu" au "baba wa zamani".

Msemo "baba wa" unaweza kumaanisha kitamathali mtu ambaye ni kiongozi wa kundi la watu wanaohusika au wenye chanzo na kitu. Kwa mfano, katika Mwanzo 4, "baba wa wale wote waishio katika mahema" inaweza kumaanisha "kiongozi wa kwanza wa ukoo wa watu wa kwanza ambao waliishi katika mahema".

Mtume Paulo alijiita kitamathali "baba" wa wale ambao aliwasaidia kuwa Wakristo kupitia kutangaza injili pamoja nao.

Mapendekezo ya Tafsiri

Unapozungumza juu ya baba na mtoto wake halisi, msemo huu unatakiwa kutafsiriwa kutumia neno la kawaida kumaanisha baba katika lugha hiyo.

"Mungu Baba" inatakiwa kutafsiriwa kutumia neno la kawaida la "baba".

Unapomaanisha mababu, msemo huu unaweza kutafsiriwa kama "babu" au "baba wa zamani".

Paulo anapomaanisha mwenyewe kitamathali kuwa baba wa waumini katika Kristo, hii inaweza kutafsiriwa kama "baba wa kiroho" au "baba katika Kristo".

Mara nyingine neno "baba" linaweza kutafsiriwa kama "kiongozi wa ukoo".

Msemo "baba wa uongo wote" unaweza kutafsiriwa kama "chanzo cha uongo wote" au "yule ambaye uongo wote hutokana".