sw_tw/bible/other/fast.md

681 B

funga

Ufafanuzi

Msemo "kufunga" una maana ya kuacha kula chakula kwa kipindi fulani, kama vile siku moja au zaidi. Mara nyingi inajumulisha kutokunywa.

Kufunga kunaweza kusaidia watu kumlenga Mungu na kuomba bila kutolewa mawazo kwa kuandaa chakula na kula.

Yesu aliwalaani viongozi wa dini wa Kiyahudi kwa kufunga kwa sababu ambazo sio sahihi. Walifunga ili kwamba wengine wafikiri kuwa wao ni watakatifu.

Mara nyingi watu walifunga kwa sababu walikuwa na huzuni sana au majonzi juu ya jambo.

Kitenzi cha "kufunga" kinaweza kutafsiriwa kama "kujizuia kula" au "kutokula".

Nomino ya "funga" inaweza kutafsiriwa kama "muda wa kutokula" au "muda wa kujizuia na chakula"