sw_tw/bible/other/family.md

757 B

familia

Ufafanuzi

Msemo "familia" una maana ya kundi la watu ambao wana uhusiano wa damu na mara nyingi hujumuisha baba, mama, na watoto wao. Mara kwa mara pia hujumuisha ndugu wengine kama babu na bibi, wajukuu, wajomba na shangazi.

Familia ya Kiebrania ilikuwa jamii ya kidini inayopitisha utamaduni kupitia ibaada na maagizo.

Mara kwa mara baba alikuwa mwenye mamlaka ya familia.

Familia pia inaweza kujumuisha watumishi, masuria, na hata wageni.

Baadhi ya lugha zina neno pana kama vile "ukoo" au "nyumba" ambayo litafaa zaidi kwa muktadha ambapo zaidi ya wazazi na watoto wanatajwa.

Msemo "familia" pia unatumika kumaanisha watu ambao wana uhusiano wa kiroho, watu kama hawa ambao ni sehemu ya familia ya Mungu kwa sababu wanmwamini Yesu.