sw_tw/bible/other/exile.md

1.0 KiB

kuhamisha, Uhamisho

Ufafanuzi

Msemo "kuhamisha" una maana ya watu waliolazimishwa kuishi mahali mbali na nchi yao ya nyumbani.

Watu mara kwa mara hutumwa uhamishoni kwa ajili ya adhabu au sababu za kisiasa.

Watu walioshindwa wanaweza kupelekwa uhamishoni katika nchi ya jeshi iliyowashinda ili kuwafanyia kazi.

"Uhamisho wa Babeli" (au "Uhamisho") ni kipindi katika historia ya Biblia ambapo raia wengi wa Kiyahudi wa eneo la Yuda walichukuliwa kutoka nyumbani mwao na kulazimishwa kuishi Babeli. Ilidumu miaka 70.

Msemo "waliohamishwa" una maana ya watu ambao wanaishi katika uhamisho, mbali na nchi yao ya nyumbani.

Mapendekezo ya Tafsiri

Msemo wa "kuhamisha" unaweza kutafsiriwa kama "kufukuza" au "kulazimisha kutoka nje" au "kuondoa".

Msemo "Uhamisho" unaweza kutafsiriwa kwa neno au msemo ambao una maana "muda ambao walifukuzwa" au "muda wa kufukuzwa" au "muda wa kulazimishwa kutokuwepo" au "kuondolewa".

Njia za kutafsiri "waliofukuzwa" zinaweza kujumuisha, "watu waliofukuzwa" au "watu ambao waliondolewa" au "watu walifukuzwa kwenda Babeli"