sw_tw/bible/other/endure.md

1.0 KiB

vumilia, uvumilivu

Ufafanuzi

Msemo "vumilia" una maana ya kudumu muda mrefu au kustahamili jambo gumu kwa uvumilivu.

Pia ina maana ya kusimama imara wakati wa mitihani kuwepo, bila kukata tamaa.

Msemo "uvumilivu" unaweza kumaanisha "subira", "ustahamilivu katika majaribu" au "kustahamili pale unapoteswa".

Faraja kwa Wakristo "kuvumilia mpaka mwisho" ni kuwaambia wamtii Yesu, hata kama hili litasababisha wao kuteseka.

"Kuvumilia mateso" pia inaweza kumaanisha "kupitia mateso".

Mapendekezo ya Tafsiri

Njia za kutafsiri msemo "vumilia" zinaweza kujumuisha "stahamili" au "kuendelea kuamini" au "kuendelea kufanya kile Mungu anachotaka ufanye" au "simama imara".

Katika baadhi ya muktadha, "kuvumilia" kunaweza kutafsiriwa kama, "kupitia jaribu" au "kupitia".

Kwa maana ya kudumu muda mrefu, msemo "vumilia" unaweza kutafsiriwa kama "kudumu" au "kuendelea". Msemo, "hatavumilia" unaweza kutafsiriwa kama, "hatadumu" au "hataendele kuishi".

Njia za kutafsiri "uvumilivu" unaweza kujumuisha "ustahamilivu" au "kuendelea kuamini" au "kubaki mwaminifu".