sw_tw/bible/other/encourage.md

764 B

tia moyo, kutia moyo

Ufafanuzi

Msemo "tia moyo" na "kutia moyo" ina maana ya kusema na kufanya mambo kusababisha mtu kuwa na faraja, matumaini, kujiamini na ujasiri.

Msemo wa kufanana ni "shawishi", ambao una maana ya kumsihi mtu kukataa tendo ambalo ni baya na badala yake kufanya mambo ambayo ni mazuri na sahihi.

Mtume Paulo na waandishi wengine wa Agano Jipya walifundisha Wakristo wajitie moyo wao kwa wao kupendana na kutumikiana.

Mapendekezo ya Tafsiri

Kulingana na muktadha, njia za kutafsiri "tia moyo" zinaweza kujumuisha, "kusihi" au "kufariji" au "kusema vitu vya upole" au "kusaidia na kuimarisha".

Msemo, "toa maneno ya faraja" una maana ya "kusema mambo ambayo yatasababisha watu wengine kujisikia kupendwa, kukubalika, na kuwezeshwa".