sw_tw/bible/other/eagle.md

595 B

tai

Ufafanuzi

Tai ni ndege mbua mkubwa sana, mwenye nguvu ambaye hula wanyama wadogo kama vile samaki, panya, nyoka na kuku.

Biblia hulinganisha kasi na nguvu ya jeshi kwa jinsi tai hupaa chini kukamata nyama yake kwa kasi na ghafla.

Isaya anasema ya kwamba wale wanaomtumaini Bwana watapaa juu kama tai afanyavyo. Hii ni lugha ya tamathali inayotumika kuelezea uhuru na nguvu ambao unakuja kutokana na kumuamini na kumtii Mungu.

Katika kitabu cha Danieli, urefu wa nywele za Mfalme Nebukadreza zililinganishwa na urefu wa manyoya ya tai, ambayo yanaweza kuwa zaidi ya sentimita 50.