sw_tw/bible/other/drinkoffering.md

871 B

sadaka ya kinywaji

Ufafanuzi

Sadaka ya kinywaji kilikuwa sadaka kwa Mungu amabyo ilihusisha kumwaga divai juu ya madhabahu. Mara kwa mara ilitolewa pamoja na sadaka ya kuteketeza na sadaka ya mazao.

Paulo anamaanisha maisha yake kama kumwagwa nje kama sadaka cha kinywaji. Hii ina maana ya kwamba aliwekwa wakfu kabisa kumtumikia Mungu na kuwaambia watu juu ya Yesu, hata kama alijua angeteseka na labda kuuwawa kwa sababu ya hiyo.

Kifo cha Yesu juu ya msalaba kilikuwa sadaka ya kinywaji ya mwisho, na damu yake ilimwagwa juu ya msalaba kwa ajili ya dhambi zetu.

Mapendekezo ya Tafsiri

Njia nyingine ya kutafsiri msemo huu unaweza kuwa, "saaka ya divai ya mizabibu".

Paulo anaposema anakuwa "anamwagwa kama sadaka" hii inaweza kutafsiriwa kama, "nimejikabidhi kufundisha ujumbe wa Mungu kwa watu, kama sadaka ya divai inavyomwagwa kabisa juu ya madhabahu".