sw_tw/bible/other/divination.md

1.0 KiB

uaguzi, mwaguzi, kutabiri, mtabiri

Ufafanuzi

Msemo "uaguzi" na "kutabiri" ina maana ya tendo la kujaribu kupata taarifa kutoka kwa roho katika ulimwengu wa rohoni. Mtu anayefanya hivi mara nyingine hujulikana kama "mwaguzi" au "mtabiri".

Katika kipindi cha Agano la Kale, Mungu aliamuru Waisraeli kutofanya uaguzi au utabiri.

Mungu hakuruhusu watu wake kutafuta taarifa kutoka kwake kutumia Urimu na Thumimu, ambayo yalikuwa mawe aliyoyatenga kutumika na makuhani wa juu kwa kusudi hilo. Lakini hakuruhusu watu wake kutafuta taarifa kupitia msaada wa roho chafu.

Waaguzi wa kipagani walitumia taratibu tofauti za kujaribu kutafuta taarifa kutoka kwenye ulimwengu wa roho. Mara zingine walichunguza sehemu za ndani za mnyama aliyekufa au kurusha mifupa ya wanyama juu ya ardhi, wakitafuta violezo ambavyo vingeweza fasiri ujumbe kutoka kwa miungu yao ya uongo.

Katika Agano Jipya, Yesu na mitume pia walikataa uaguzi, uchawi, ulozi na mazingaombwe. Matendo haya yote yalihusisha matumizi ya nguvu kutoka roho chafu na yanalaaniwa na Mungu.