sw_tw/bible/other/detestable.md

1.1 KiB

chukiza, chukia

Ufafanuzi

Msemo "chukiza" unaelezea jambo ambalo linapaswa kutopendwa na kukataliwa. "Kuchukia" kitu ina maan ya kutokipenda kabisa.

Mara nyingi Biblia huzungumzia kuhusu kuchukia uovu. Hii ina maana kuchukia uovu na kuukataa.

Mungu alitumia neno "chukiza" kuelezea matendo maovu ya wale waliomwabudu miungu ya uongo.

Waisraeli waliamriwa "kuchukia" matendo ya dhambi, na kinyume na maadili ambayo baadhi ya makundi ya watu majirani waliyafanya.

Mungu aliyataja matendo yote ya uasherati kuwa "chukizo".

Uaguzi, uchawi, na sadaka za mtoto yote yalikuwa "chukizo" kwa Mungu.

Msemo "chukizo" unaweza kutafsiriwa kama "uovu mbaya" au "inayochukiza" au "inayostahili kukataliwa".

Inapotumika na kiumbe takatifu "chukizo kwa" waovu, hii inaweza kutafsiriwa kama "kuchukuliwa kutotamanika kwa" au "kutokuwa na ladha" au "kukataliwa na"

Mungu aliwaambia Waisraeli "kuchukia" aina kadhaa ya wanyama ambao Mungu alitamka kuwa "wachafu" na kutofaa kwa chakula. Hii inaweza kutafsiriwa kama "kuchukia kwa uzito" au "kukataa" au "kuchukua kama kutokubalika".