sw_tw/bible/other/destiny.md

1.3 KiB

takdiri, majaliwa, jaliwa

Ufafanuzi

Msemo wa "takdiri" una maana ya kile kitakachotokea kwa watu hapo baadaye. Kama mtu ana "takdiri" ya jambo, ina maana ya kwamba kile mtu huyo atafanya hapo baadaye kimepangwa na Mungu.

Mungu anapopanga taifa kupatwa na ghadhabu, hii ina maana ya kwamba ameamua au kuchagua kuwaadhibu taifa hilo kwa sababu ya dhambi yao.

Yuda alikuwa na "takdiri" ya kuangamizwa, ina maana ya kwamba Mungu aliamua ya kwamba Yuda angeangamizwa kwa sababu ya kuasi kwake.

Kila mtu ana takdiri ya mwisho, ya milele, moja wapo mbinguni au jehanamu.

Pale mwandishi wa Mhubiri anaposema ya kwamba kila mtu takdiri yake inafanana, anamaanisha ya kwamba kila mtu hatma yake atakufa.

Mapendekezo ya Tafsiri

Msemo "kupangwa kwa ghadhabu" unaweza pia kutafsiriwa kama "kuamua ya kwamba utaadhibiwa" au "kuamuliwa ya kwamba utapitia ghadhabu yangu".

Msemo wa kitamathali, "wana takdiri ya upanga" inaweza kutafsiriwa kama, "Mungu ameamua ya kwamba wataangamizwa na adui zake ambao watawaua kwa upanga" au "Mungu ameamua ya kwamba adui wao watawaua kwa upanga".

Msemo, "una takdiri ya" inaweza kutafsiriwa kutumia msemo kama, "Mungu ameamua ya kwamba utakuwa"

Kutegemea na muktadha, "takdiri" inaweza kutafsiriwa kama "hitimisho la mwisho" au "kitakachotokea mwishoni" au "kile alichoamua Mungu kitatokea"