sw_tw/bible/other/declare.md

873 B

tamka, tamko

Ufafanuzi

Msemo wa "tamka" au "tamko" una maana ya kutoa kauli maalumu kwa umma, mara nyingi kusisitiza jambo.

"Tamko" halisisitizi umuhimu tu wa kile kinachotamkwa, lakini inavuta nadhari kwa yule anayetoa tamko hilo.

Kwa mfano, katika Agano la Kale, ujumbe kutoka kwa Mungu mara nyingi hutanguliwa na "tamko la Yahwe" au "hivi ndivyo Yahwe asemavyo". Msemo huu unasisitiza ya kwamba ni Yahwe mwenyewe anayesema hivi. Ukweli ya kwamba ujumbe unatoka kwa Yahwe unaonyesha jinsi ujumbe ulivyo na umuhimu.

Mapendekezo ya Tafsiri

Kulingana na muktadha, "tamka" inaweza pia kutafsiriwa kama "tangaza" au "eneza wazi" au "sema kwa nguvu" au "tamka kwa kishindo".

Msemo "tamko" unaweza kutafsiriwa kama, "kauli" au "tangazo".

Msemo, "hili ni tamko la Yahwe" linaweza kutafsiriwa kama, "hivi ndivyo Yahwe anavyotamka" au "hivi ndivyo Yahwe anavyosema".