sw_tw/bible/other/death.md

1.3 KiB

kifo, kufa, mfu

Ufafanuzi

Msemo huu unatumika kumaanisha vyote kifo cha kimwili na kiroho. Kimwili, ina maana ya mwili wa kihalisia wa mtu kukoma kuishi. Kiroho, ina maana ya wenye dhambi kutengwa na Mungu mtakatifu kwa sababu ya dhambi yao.

Mapendekezo ya Tafsiri

Kutafsiri msemo huu, ni vyema kutumia neno la kila siku au usemi ambao una maana ya kifo katika lugha husika.

Katika baadhi ya lugha, "kufa" inaweza kuelezwa kama "kutokuishi". Msemo "kufa" unaweza kutafsiriwa kama "kutokuwa hai" au "kutokuwa na uhai wowote" au "kutokuishi".

Lugha nyingi zinatumia msemo wa tamathali kuelezea kifo, kama "kuondoka" kwa Kiingereza. Ila katika Biblia ni bora kutumia msemo wa moja kwa moja kwa ajili ya kifo ambao unatumika kila siku katika lugha.

Katika Biblia, uhai na kifo wa kimwili mara kwa mara hulinganishwa na uhai na kifo cha kiroho. Ni muhimu katika tafsiri kutumia neno moja au msemo kwa ajili kifo cha kimwili na kifo cha kiroho.

Katika baadhi ya lugha inaweza kuwa wazi zaidi kusema, "kifo cha kiroho" ambapo muktadha unahitaji maana hiyo. Watafsiri wengine wanaweza kuhisi ni bora kusema, "kifo cha kimwili" katika muktadha ambapo unalinganishwa na kifo cha kiroho.

Msemo wa "wafu" ni kivumishi chenye maana ya watu waliokufa. Baadhi ya lugha zitatafsiri hili kama, "watu waliokufa" au "watu ambao wamekufa"