sw_tw/bible/other/darkness.md

1.1 KiB

Giza

Ufafanuzi

Msemo "giza" una maana ya kutokuwepo kwa nuru. Kuna maana kadhaa za kitamathali za msemo huu:

Kama sitiari, "giza" ina maana ya "uchafu" au "uovu" au "upofu wa kiroho".

Pia ina maana ya jambo lolote linalohusu dhambi au uharibifu wa maadili.

Msemo, "mamlaka ya giza" una maana ya kila kilicho kiovu na kinachotawaliwa na Shetani.

Msemo "giza" unaweza pia kutumika kama sitiari ya kifo.

Watu wasiomjua Mungu wanasemekana kuwa "wanaishi gizani", ambayo ina maana hawaelewi au hawatenda haki.

Mungu ni nuru (utakatifu) na giza (uovu) haliwezi kushinda nuru hiyo.

Mahali pa adhabu kwa wale wanaomkataa Mungu mara nyingi hujulikana kama "giza la nje".

Mapendekezo ya Tafsiri

Ni bora kutafsiri msemo huu kihalisia, kwa neno la lugha ya mradi ambalo lina maanisha kutokuwepo kwa nuru. Huu unaweza kuwa msemo wenye maana ya giza la chumba ambalo halina mwanga au wakati wa siku ambapo hakuna mwanga.

Kwa matumizi ya kitamathali, ni muhimu kuweka picha ya giza kwa kutofautisha na mwanga, kama njia ya kuelezea uovu na udanganyifu kulinganisha na wema na ukweli.

Kutegemea na muktadha, njia zingine za kutafsiri hili zaweza kuwa, "giza la usiku"