sw_tw/bible/other/cow.md

658 B

Ng'ombe, fahali, ndama, mifugo

Ufafanuzi

Mifugo ni kundi kubwa la wanyama wenye miguu minne wanaokula majani na hufugwa kwa ajili ya maziwa na nyama.

  • Ng'ombe dume huitwa fahali na ng'ombe mdogo huitwa ndama.
  • Mara nyingine ng'ombe hutumika kuwakilisha aina zote za mifugo.
  • Katika tamaduni zingine ng'ombe hubadilishwa na bidhaa katika biashara. Mara nyingine hutumika kama zawadi itolewayo kwa wazazi wa binti na mwanaume anayetaka kumuoa.
  • Katika Biblia Wayahudi walitumia mifugo kwa ajili ya dhabihu hasa ng'ombe mwekundu.
  • Ng'ombe mwekundu ni ng'ombe ambaye hajazaa bado.
  • Pia kuna ng'ombe dume ambaye hutumika katika shughuli za kilimo.