sw_tw/bible/other/bronze.md

668 B

shaba

Ufafanuzi

Neno "shaba" linamaanisha aina ya madini yatengenezwayo kwa kuyeyusha kwa pamoja metali, shaba nyekundu na bati. Ina rangi nyeusi inayoelekea njano, nyekundu kiasi.

  • Shaba huzuia kutu na kipitisho kizuri cha joto
  • Hapo kale, shaba ilitumika kutengeneza dhana, silaha, madhabahu, vyungu, silaha za askari na vitu vingine.
  • Vifaa vingi vya kujengea hema la kukutania na hekalu vilikuwa vimetengenezwa kwa shaba.
  • Kwa kawaida vinyago vya miungu ya uongo vilitengenezwa kwa madini ya shaba.
  • Dhana za shaba zilitengenezwa baada ya kuyeyusha madini ya shaba na kisha kuyamimina katika chombo cha kutengenezea. Mchakato huu uliitwa "kutupa."