sw_tw/bible/other/12tribesofisrael.md

818 B

Makabila kumi na mbili ya Israeli

Ufafanuzi

Makabila kumi na mbili inamaanisha watoto kumi na mbili wa Yakobo na uzao wao. Yakobo alikuwa mjukuu wa Abrahamu. Baadae Mungu alibadili jina lake na kumuita Israeli. Haya ndio majina ya makabila ya Israeli; Rubeni, Simoni, Lawi, Yuda, Naftali, Gadi, Asheri, Isakari, Zabuloni, Yusufu na Benjamini. Kizazi cha Lawi hakikurithi nchi ya Kaanani kwa sababu lilikuwa kabila la Kikuhani waliotengwa kumtumikia Mungu na watu wake. Yusufu alipokea urithi wa ardhi mara mbili ambapo aliwapatia watoto wake wawili Efraimu na Manase. Kuna mahali pengine kwenye Biblia orodha ya makabila kumi na mbili yamenukuliwa tofauti. Sehemu nyingine Lawi, Yusufu na Dani hawakuwekwa kwenye orodha na sehem nyingine watoto wawili wa Yusufu Efraimu na Manase wamewekwa kwenye orodha.