sw_tw/bible/names/stephen.md

862 B

Stefano

Ufafanuzi

Stefano anajulikana kama Mkristo wa kwanza kuuawa, sababu ya imani yake kwa Yesu. Maisha yake na kifo yameandikwa kwenye kitabu cha Matendo.

  • Stefano alichaguliwa na Kanisa la awali la Yerusalemu kutumikia Wakristo kama shemasi kuwapa chakula wajane na wengine Wakristo wenye maitaji.
  • Baadhi ya Wayahudi walimshtumu kwa uongo Stefano kuzungumza dhidi ya Mungu na dhidi ya sheria ya Musa.
  • Stefano kwa ujasiri alisema ukweli kuhusu Yesu Mesiya, kwa kuanza na historia ya matendo ya Mungu kwa Waisraeli.
  • Viongozi wa Wayahudi walikasirika na kumuua Stefano kwa kumpiga mawe hadi kufa nje ya mji.
  • Kifo chake kilishuhudiwa na Sauli wa Tarso, baade kuwa mtume Paulo.
  • Stefano anajulikana pia kwa maneno yake ya mwisho kabla ya kufa: Bwana, tafadhali usihesabu dhambi hii dhidi yao," iliyo onyesha upendo aliyo kuwa nao kwa wengine.