sw_tw/bible/names/phinehas.md

667 B

Finehasi

Ufafanuzi

Finehasi ni jina la watu wawili katika agano la kale.

  • Mmoja wa wajukuu wa Haruni alikuwa kuhani aliyeitwa finehasi aliyepinga kwa nguvu kuabudu miungu ya uongo.
  • Finehasi aliwaokoa Waisraeli toka kwenye pigo ambalo bwana alilituma ili kuwaadhibu kwa kuwaoa wanawake wa Midiani na kuabudu miungu yao ya uongo.
  • Katika matukio mbali mbali Finehasi alikwenda na jeshi la Israeli kuwapiga Wamidiani.
  • Finehasi mwingine aliyetajwa kwenye agano la kale alikuwa mmoja wa wana waovu wa kuhani Eli katika kipindi cha nabii Samweli.
  • Finehasi na kaka yake Hofini waliuawa kipindi ambacho Wafilisti walivamia Israeli na kuiba sanduku la agano.