sw_tw/bible/names/paran.md

561 B

Parani

Ufafanuzi

Parani ni jangwa lililopo mashariki mwa Misri na kusini mwa nchi ya Kanaani. Pia kulikuwa na mlima Parani ambalo yaweza kuwa jina lingine la mlima Sinai.

  • Mtumwa Hagari na mtoto wake walikwenda kuishi katika jangwa la Parani baada ya Sara kumuamuru Abrahamu amfukuze.
  • Musa alipowaongoza Waisraeli kutoka Misri walipitia jangwa la Parani.
  • Ilikuwa toka Kadesh-barnea kupitia jangwa la Parani ambalo Musa aliwatuma wapelelezi kumi na mbili kupeleleza nchi ya Kanaani na kuleta ripoti.
  • Jangwa la Sini lilikuwa kaskazini mwa Parani.