sw_tw/bible/names/levite.md

673 B

Mlawi, Lawi

Ufafanuzi

Lawi alikuwa mmoja wa wana kumi na mbili wa Yakobo, au Israeli. Neno "Mlawi" inamaanisha mtu aliyemmoja wa kabila la Israeli ambalo babu yao alikuwa Lawi.

Walawi walihusika na kulitunza hekalu na kuendesha taratibu za kidini, zikiwemo kutoa sadaka na maombi. Makuhani wote wa Kiyahudi walikuwa Walawi, wazawa wa Lawi na sehemu ya kabila la Lawi. (Ingawa Walawi wote hakuwa makuhani.) Makuhani wa Kilawi walitengwa na kuwekwa wakfu kwa kazi maalum ya kumtumikia Mungu hekaluni. Wanaume wengine wawili wenye jina "Lawi" walikuwa mababu wa Yesu na majina yao yako kwenye ukoo katika injili ya Luka. Mwanafuzi wa Yesu, Mathayo, pia aliitwa Lawi.