sw_tw/bible/names/kingdomofisrael.md

786 B

ufalme wa Israeli

Ufafanuzi

Usemi "ufalme wa Israeli" unamaanisha sehemu ya kaskazini mwa taifa la Israeli wakati makabila kumi na mbili ya Israeli yalipogawanyika katika falme mbili baada ya Sulemani kufa.

Ufalme wa Israeli wa kaskazini ulikuwa na makabila kumi na ufalme wa Yuda ulikuwa na makabila mawili. Mji mkuu wa ufalme wa Israeli ulikuwa Samaria. Ilikuwa kama kilomita 50 kutoka Yerusalemu, mji mkuu wa Yuda. Wafalme wote wa ufalme wa Israeli walikuwa waovu. Waliwashawishi watu kutumikia sanamu na miungu ya uongo. Mungu aliwatuma Waashuri kuvamia taifa la Israeli. Waisraeli wengi walikamatwa na kupelekwa kuishi Ashuru. Waashuri waliwaleta wageni kuishi miongoni mwa watu waliobaki wa Israeli. wageni hawa waliowana na Waisraeli, na uzao wao ukawa watu wa Samaria.