sw_tw/bible/names/kedar.md

668 B

Kedari

Ufafanuzi

Kedari lilikuwa jina la mwana wa pili wa Ishmaeli. Lilikuwa pia jina la mji muhimu ambalo linawezekana kuwa liliitwa baada ya huyo mwanamme

Mji wa Kaderi inapatikana katika eneo la kaskazini la Arabia karibu na mpaka wa kusini ya Filisti. Katika nyakati za Biblia, palikuwa panajulikana kwa ukuu na uzuri wake. Wazawa wa Kaderi waliunda kundi kubwa la watu linaloitwa "Kaderi." Usemi "hema za Kedari nyeusi" inamaanisha hema za nywele nyeusi za mbuzi ambamo watu wa Kaderi waliishi. Watu hawa walifuga kondoo na mbuzi. Pia walitumia ngamia kwa kusarifishia vitu. Katika Biblia, usemi "utukufu wa Kedari" inamaanisha ukuu wa mji na watu wake.