sw_tw/bible/names/judassonofjames.md

611 B

Yuda mwana wa Yakobo

Ufafanuzi

Yuda mwana wa Yakobo alikuwa mmoja wa mitume kumi na mbili wa Yesu. Huyu hakuwa Yuda Iskariote.

Mara nyingi katika Biblia, wanaume wenye majina ya kufanana hutofautishwa kwa kutaja walikuwa wana wa nani. Hapa Yuda anatajwa kama "mwana wa Yakobo." Mwanamme mwingine aitwaye Yuda alikuwa ndugu yake Yesu. Kitabu cha Agano Jipya cha"Yuda" kinawezekana kuwa kimeandikwa na ndugu yake Yesu Yuda, kwa kuwa anajitambulisha kama "ndugu yake Yakobo." Yakobo alikuwa ndugu mwingine wa Yesu. Inawezekana kuwa kitabu cha Yuda kiliandikwa na mwanafunzi wa yesu, Yuda mwana wa Yakobo.