sw_tw/bible/names/joshua.md

1.1 KiB

Yoshua

Ufafanuzi

Kuna Waisraeli kadhaa kwenye Biblia waitwao Yoshua. Anayejulikana zaidi ni Yoshua mwana wa Nuni aliyekuwa msaidizi wa Musa na baadaye kuwa kiongozi muhimu wa watu wa Mungu.

Yoshua alikuwa mmoja wa wapelelezi kumi na mbili amabo Musa aliwatuma tafiti nchi ya ahadi. Pamoja na Kalebu, Yoshua aliwasihi watu wa Israeli watu kutii amri ya Mungu kuingia nchi ya ahadi na kuwashinda Wakanaani. Miaka mingi baadaye, baada ya Musa kufa, Mungu alimchagua Yoshua kuwaongoza watu Waisraeli kwenda nchi ya ahadi. Katika mapambano ya kwanza na maarufu zaidi dhidi ya Wakanaani, Yoshua aliwaongoza Waisraeli kuuangamiza mji wa Yeriko. Kitabu cha Agano la Kale cha Yoshua kinaelezea jinsi Yoshua alivyowaongoza Waisraeli katika kuichukua mamlaka nchi ya ahadi na jinsi alivyopanga sehemu tofauti za nchi kwa kila kabila la Israeli kuishi. Yoshua mwana wa Yosadaki anatajwa katika vitabu vya Hagai na Zekaria; alikuwa kuhani mkuu aliyesaidia kujenga tena kuta za Yerusalemu. Kuna wanaume kadhaa wengine waitwao Yoshua waliotajwa katika koo na sehemu zingine katika Biblia.