sw_tw/bible/names/jonathan.md

496 B

Yonathani

Ufafanuzi

Yonathani ni jina la angalau wanaume kumi katika Agano la Kale. Jina linamaanisha "Yahwe ametoa."

Rafiki wa karibu wa Daudi , Yonathani, ndiye anayejulikna zaidi katika Biblia kwa hili jina. Yonathani alikuwa mwana kwanza wa mfalme Sauli. Yonathani wengine waliotajwa katika Agano la Kale ni pamoja na: uzao wa Musa, mpwa wa mfalme Daudi, makuhani kadhaa, akiwemo mwana wa Abiathari; na mwandishi wa Agano la Kale ambaye nyumba yake ilitumika kumfunga nabii Yeremia.