496 B
496 B
Yonathani
Ufafanuzi
Yonathani ni jina la angalau wanaume kumi katika Agano la Kale. Jina linamaanisha "Yahwe ametoa."
Rafiki wa karibu wa Daudi , Yonathani, ndiye anayejulikna zaidi katika Biblia kwa hili jina. Yonathani alikuwa mwana kwanza wa mfalme Sauli. Yonathani wengine waliotajwa katika Agano la Kale ni pamoja na: uzao wa Musa, mpwa wa mfalme Daudi, makuhani kadhaa, akiwemo mwana wa Abiathari; na mwandishi wa Agano la Kale ambaye nyumba yake ilitumika kumfunga nabii Yeremia.