sw_tw/bible/names/joash.md

769 B

Yoashi

Ufafanuzi

Yoashi lilikuwa jina la watu kadhaa katika Agano la Kale.

Yoashi mmoja alikuwa baba wa mkombozi mmoja wa Israeli, Gideoni. Mwanamme mwingine aliyeitwa Yoashi alikuwa uzao wa mwana wa mwisho wa Yakobo, Benyamini. Yoashi anayejulikanai vizuri zaidi alikuwa mfalme wa Yuda akiwa na umri wa miaka saba. Alikuwa mwana wa Ahazia, mfalme wa Yuda aliyeuwawa. Yoashi alipokuwa mtoto mdogo, shangazi yake alimuokoa kuuliwa kwa kumficha hadi alipokuwa na umri wa kutosha kufanywa mfalme. Mfalme Yoashi alikuwa mfalme mzuri ambaye mwanzoni alimtii Mungu. Ila hakutoa sehemu zilizo inuka na Waisreali wakaanza tena kuabudu sanamu. Mfalme Yoashi alitawala Yuda wakati wa baadhi ya miaka mfalme Yehoashi alipotawala Israeli. Walikuwa wafalme wawili tofauti.