sw_tw/bible/names/jacob.md

914 B

Yakobo, Israeli

Ufafanuzi

Yakobo alikuwa pacha mdogo aliyekuwa mwana wa Isaka na Rebeka.

Jina la Yakobo linamaanisha "anakamata kisigino" ambao ni usemi unaomaanisha, "hudanganya." Wakati yakobo alipozaliwa, alikuwa akishilia kisigino cha pacha wake Esau. Miaka mingi baadaye, Mungu alibalisha jina la Yakobo kuwa "Israeli," inayomaanisha, "anashindana na Mungu." Yakobo alikuwa mjanja na muongo. Alipata njia ya kupata baraka za mwana wa kwanza na kurithi haki kutoka kwa kaka yake, Esau. Esau alikasirika na kupanga kumuua, kwa hiyo Yakobo akaondoka nchini mwake. Lakini baada ya miaka Yakobo alirudi na wake zake na watoto katika nchi ya Kanaani ambamo Esau alikuwa akiishi, na familia zao ziliishi kwa amani zikiwa jirani. Yakobo alikuwa na wana kumi na mbili. Uzao wao ukawa makabila kumi na mbili ya Israeli. Mwanaume tofauti aitwaye Yakobo ameorodheshwa kama baba wa Yusufu katika ukoo wa Mathayo.