sw_tw/bible/names/ishmael.md

690 B

Ishmaeli

Ufafanuzi

Ishmaeli alikuwa mwana wa Abrahamu na mtumwa wa Kimisri Hagai. Kuna wana kadhaa pia katika Agano la Kale wanaoitwa Ishmaeli.

Jina "Ishmaeli" linamaanisha, "Mungu husikia." Mungu aliahidi kumbariki mwana wa Abrahamu, Ishmaeli, lakini hakuwa mwana ambaye Mungu aliye ahidi kuweka agano lake naye. Mungu alimlinda Hagai na Ishmaeli walipotumwa jangwani. Wakati Ishmaeli alipokuwa akiishi katika jangwa la Parani, alimuoa mwanamke wa Misri. Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa afisa wa jeshi kutoka Yuda aliyeongoza kundi la wanaume kumua gavana aliyeteuliwa na mfalme wa Kibabeli, Nebukadreza. Pia kuna wanaume wengine wanne walioitwa Ishmaeli katika Agano la Kale.