sw_tw/bible/names/isaac.md

776 B

Isaka

Ufafanuzi

Isaka alikuwa mwana pekee wa Abrahamu na Sara. Mungu aliwaahidi kuwapa mwana wa kiume ingiwa walikuwa wazee sana.

Jina "Isaka" linamaanisha "kicheko." Mungu alipomuambia Abrahamu kuwa Sara atazaa mwana wa kiume, Abrahamu alicheka kwa sababu wote walikuwa wazee sana. Baada ya muda, Sara pia alicheka aliposikia taarifa hii. Lakini Mungu alitimiza ahadi yake na Isaka alizaliwa kwa Abrahamu na sara katika uzee wao. Mungu alimuambia Abrahamu kuwa agano alilofanya na Abrahamu itakuwa pia ya Isaka na vizazi vyake milele. Wakati Isaka alikuwa kijana, Mungu aliijaribu imani ya Abrahamu kwa kumuamuru kumtoa isaka kama sadaka. Mwana wa Isaka, Yakobo, alikuwa na wana kumi na mbili ambao uzao wao baadaye ukawa makabila kumi na mbili ya taifa la Israeli.