sw_tw/bible/names/horeb.md

836 B

Horebu

Ufafanuzi

Mlima Horebu ni jina jingine la mlima Sinai, mahali ambapo Mungu alimpa Musa vipande vya mawe vya amri kumi za Mungu. Mlima Horebu huitwa Mlima wa Mungu Musa aliiona kichaka kilichokuwa kinawaka moto wakati akichunga kondoo katika mlima Horebu. Katika mlima Horebu, Mungu alifunua agano lake kwa Waisraeli kwa kuwapa vipande vya mawe vilivyo na Amri juu yake. Ni mahali ambapo Mungu alimwambia Musa kuupiga mwamba ili maji yatoke kwa ajili ya waisraeli katika kipindi walichokuwa wanazunguka jangwani. Sehemu maalumu ulipo mlima huu haijulikani, huenda ni sehemu ya kusini ambayo kwa sasa inajulikana kama 'Penisula ya Sinai Inawezekana kuwa Horebu lilikuwa ni jina kamili la mlima na kwamba Mlima Sinai ina maana ya milima ya Sinai kwa kurejelea ukweli kwamba Mlima Horebu ulikuwa katika jangwa la Sinai.