sw_tw/bible/names/hivite.md

479 B

Mhivi

Ufafanuzi

Wahivi walikuwa ni moja kati ya makundi saba ya watu walioishi katika nchi ya Kanaani. Kama ilivyokuwa kwa makundi yote, Wahivi walikuwa ni uzao wa Kanaani, aliyekuwa ni mjukuu wa Nuhu. Shekemu mhivi alimbaka Dina, binti wa Yakobo na kaka zake na Dina walilipiza kisasi kwa kuwauwa Wahivi wengi. Katika kipindi ambacho Yoshua aliwaongoza waisraeli kuiteka nchi ya Kanaani, Waisraeli walidanganywa na kufunga mkataba na Wahivi badala ya kuwaangamiza.