sw_tw/bible/names/hezekiah.md

632 B

Hezekia

Ufafanuzi

Hezekia alikuwa ni mfalme wa 13 wa ufalme wa Yuda. Alikuwa ni mfalme aliyemtumaini Mungu na kumtii. Tofauti na baba yake, Ahazi aliyekuwa mfalme mwovu, Mfalme Hezekia alikuwa ni mfalme mzuri aliyeharibu maeneo yote ya ibada ya miungu katika Yuda. Wakati Hezekia alipougua na alipokuwa karibu kufa, alimwomba Mungu sana ili alinde na kuhifadhi maisha yake. Mungu alimponya na alimruhusu kuishi miaka 15 zaidi. Mungu alifanya muujiza kwa Hezekia kwa kurudisha muda nyuma. Mungu alijibu maombi ya Hezekia kwa kuwaokoa watu wake kutoka mikononi mwa Mfalme Senakaribu wa Siria, aliyekuwa akiwashambulia.