sw_tw/bible/names/herodantipas.md

688 B

Herode Antipa

Ufafanuzi

Katika kipindi kirefu cha maisha ya Yesu, Herode Antipa alikuwa ni mtawala wa Dola ya Kirumi iliyojumuisha jimbo la Galilaya. Antipa mara nyingine alitajwa kama 'Mfalme" kama alivyokuwa baba yake, Herode Mkuu, ingawa hakuwa mfalme kweli. Herode Antipa alitawala robo au moja ya nne ya Dola ya Kirumi na hivyo aliitwa Herode 'Tetraki' yaani mkuu wa mkoa. Antipa ni 'Herode' aliye Yohamuru Yohana mbatizaji auawe kwa kukatwa kichwa. Alikuwa ni Herode Antipa pia aliyemwuuliza Yesu maswali kabla ya kusulubiwa kwake. Maherode wengine katika Agano Jipya walikuwa ni mtoto wa Antipa (Agripa) na mjukuu ( Agripa wa pili) aliyetawala kipindi cha mitume.