sw_tw/bible/names/gideon.md

599 B

Gideoni

Ufafanuzi

Gideoni alikuwa mwanamume wa Kiisraeli ambaye aliinuliwa na Mungu kuwakomboa Waisraeli kutoka kwa adui zao.

Katika kipindi ambacho Gideoni aliishi, kundi la watu lijulikanalo kama Midiani waliendelea kuwashambulia Waisraeli na kuangamiza mazao yao.

Ingawa Gideoni aliogopa, Mungu alimtumia kuwaongoza Waisraeli kupigana dhidi ya Midiani na kuwashinda.

Gideoni pia alimtii Mungu kwa kuangusha madhabahu chini ya miungu wa uongo wa Baali na Ashera.

Hakuwaongoza tu watu katika kuwashinda adui zao lakini pia aliwatia moyo kutii na kumwabudu Yahwe, Mungu mmoja wa ukweli.