sw_tw/bible/names/galilee.md

457 B

Galilaya, Mgalilaya

Ufafanuzi

Galilaya ni eneo la kaskazini ya Israeli, kaskazini ya Samaria. "Mgalilaya" alikuwa mtu ambaye aliishi Galilaya.

Galilaya, Samaria, na Yudea ilikuwa miji mitatu ya msingi ya Israeli wakati wa Agano Jipya.

Galilaya imepakana upande wa mashariki na ziwa kubwa liitwalo "Ziwa la Galilaya".

Yesu alikua na kuishi katika mji wa Nazareti Galilaya.

Miujiza mingi na mafundisho ya Yesu yalifanyika katika eneo la Galilaya.