sw_tw/bible/names/gabriel.md

741 B

Gabrieli

Ufafanuzi

Gabrieli ni jina la mmoja wa malaika wa Mungu. Anatajwa kwa majina kadhaa, kote katika Agano la kale na Jipya.

Mungu alimtuma Gabrieli kumwambia nabii Danieli maana ya maono aliyoyaona. Muda mwingine, Danieli alipokuwa akiomba, malaika Gabrieli alipaa kwake na kutabiri kuhusu kile kitakachotokea hapo baadaye. Danieli alimfafanua kama "mwanamume". Katika Agano Jipya inaandikwa ya kwamba Gabrieli alitokana na Zakaria kutabiri ya kwamba mke wake mzee Elizabeti angepata mwana wa kiume, Yohana. Miezi sita baada ya hapo, Gabrieli alitumwa kwa Mariamu kumwambia ya kwamba Mungu angemuwezesha kwa miujiza kupata mimba ya mtoto amabye angekuwa "Mwana wa Mungu". Gabrieli alimwambia Mariamu kumuita mwanawe "Yesu" .