sw_tw/bible/names/eve.md

433 B

Hawa

Ufafanuzi

Hili lilikuwa jina la mwanamke wa kwanza. Jina lake linamaanisha "uhai" au "kuishi".

Mungu alimuumba Hawa kutoka kwa ubavu ambao aliuchukua kutoka kwa Adamu.

Hawa aliumbwa kuwa "msaidizi" wa Adamu. Alikuja kando ya Adamu kumsaidia katika kazi ambayo Mungu aliwapa kufanya.

Hawa alijaribiwa na Shetani (kwa mfano wa nyoka) na alikuwa wa kwanza kufanya dhambi kwa kula tunda ambalo Mungu aliwaambia kutokula.