sw_tw/bible/names/ethiopia.md

776 B

Ethiopia, Mtu wa Ethiopia

Ufafanuzi

Ethiopia ni nchi katika Afrika iliyo kusini mwa Misri mpakana mwa Mto wa Naili magharibi na katika Bahari ya Shamu mashariki. Mtu kutoka Ethiopia na "mtu wa Ethiopia".

Ethiopia ya zamani ilikuwa kusini mwa Misri na ilijumuisha nchi ambayo kwa sasa ni sehemu ya baadhi ya nchi za Afrika, kama Sudani, Ethiopia ya sasa, Somalia, Kenya, Uganda, Afrika ya Kati na Chadi.

Katika Biblia, Ethiopia mara nyingine huitwa "Kushi" au "Nubia".

Nchi za Ethiopia ('Kushi') na Misri mara nyingine hutajwa pamoja katika Biblia, labda kwa sababu zilikuwa karibu na nyenzake na watu wake yawezekana walikuwa na mababu wa kufanana.

Mungu alimtuma Filipo mwinjilisti katika jangwa ambapo alisambaza habari njema kuhusu Yesu na towashi wa Ethiopia.