sw_tw/bible/names/engedi.md

565 B

Engedi

Ufafanuzi

Engedi ni jina la mji katika nyika ya Yuda kusini mashariki mwa Yerusalemu.

Engedi ilikuwa mahali mwa ukingo wa magharibi wa Bahari ya Chumvi.

Sehemu ya jina lake, "chemichemi" ina maana ya chemichemi ya maji ambayo inatiririka chini kutoka kwenye mji hadi baharini.

Engedi ilijulikana kwa kuwa na mashamba ya mizabibu mizuri na ardhi yenye rutuba nyingine, yawezekana kutokana na mwendelezo wa umwagiliaji kutoka kwa chemichemi ya maji.

Kulikuwa na ngome katika Engedi ambayo Daudi alitoroka kule alipokuwa akifukuzwa na Mfalme Sauli.