sw_tw/bible/names/dan.md

555 B

Dani

Ufafanuzi

Dani alikuwa mwana wa tano wa Yakobo na alikuwa mmoja wa makabila kumi na mawili ya Israeli. Eneo lililokaliwa na kabila la Dani sehemu ya kaskazini ya Kaanani pia lilipatiwa jina hili.

Katika kipindi cha Abrahamu, kulikuwa na mji ulioitwa Dani uliokuwa magharibi mwa Yerusalemu.

Miaka ya baadaye, katika kipindi ambapo taifa la Israeli lilipoingia katika nchi ya ahadi, mji tofauti ulioitwa Dani ulikuwa kama maili 60 kaskazini mwa Yerusalemu.

Msemo "Wadani" una maana ya vizazi vya Dani, ambao pia ni wanajumuiya wa ukoo wake.