sw_tw/bible/names/baruch.md

501 B

Baruku

Ufafanuzi

Baruku ni jina la watu kadhaa katika Agano la Kale.

  • Baruku wa kwanza (mwana wa Zabeli) alifanya kazi ya Nehemia kujenga upya kuta za Yerusalemu.
  • Lakini pia katika nyakati za Nehemia, Baruku mwingine (mwana wa Kol-Hoze) alikuwa miongoni mwa viongozi walioishi Yerusalemu baada ya kuta zake kujengwa.
  • Baruku mwingine (mwana wa Neria) alikuwa mhudumu wa nabii Yeremia, kwa kumsaidia kazi mbalimbali kama vile kuandika jumbe Mungu alizompa Yeremia na kisha kuwasomea watu.