sw_tw/bible/names/babylon.md

14 lines
1.0 KiB
Markdown

# Mji wa Babeli
## Ufafanuzi
Mji wa Babeli ulikuwa makao makuu wa jimbo la Babeli ya kale, ambao pia ulikuwa sehemu ya Himaya ya Babeli.
* Babeli ulikuwa kandokando ya Mto Frati, katika eneo ambalo mnara wa Bebeli ulikuwa umejengwa mamia ya miaka iliyokuwa imepeita.
* Wakati mwingine jina "Babeli" linarejerea Himaya yote ya Babeli. Kwa mfano, "mfalme wa Babeli alitawala himaya yote ya Babeli, siyo mji tu.
* Watu wa Babeli walikuwa wenye nguvu walioishambuli Yuda na kuwapeleka watu katika uhamisho huko Babeli kwa miaka 70.
* Sehemu yake iliitwa "Ukalidayo" na watu walioishi pale waliitwa "Wakalidayo." Matokeo yake neno "Ukalidayo mara kwa mara lilitumika kurejerea Babeli.
* Katika Agano Jipya, neno "Babeli" wakati mwingine linatumika kama sitiari kurejerea maeneo, watu, na vitu vya kufikirika viusianishwavyo na ibada ya sanamu na tabia nyingine za dhambi.
* Kirai "Babeli Mkuu" au "Babeli mji mkuu" kisitiari inarejerea kwa mji au taifa kubwa, tajiri, na lenye dhambi, kama ulivyokuwa mji wa kale wa Babeli.