sw_tw/bible/names/asaph.md

641 B

Asafu

Ufafanuzi

Asafu alikuwa kuhani wa Kilawi na mtaalamu wa muziki aliyetunga mziki wa Zaburi ya mfalme Daudi. Pia aliandika zaburi yake mwenyewe.

  • Asafu alichaguliwa na mfalme Daudi kuwa moja ya wanamuziki watatu waliokuwa wakitengeneza nyimbo za kuabudu hekaluni. Baadhi ya nyimbo hizi zilikuwa unabii.
  • Asafu aliwafundisha watoto wake na wakabeba majukumu ya kutumia vyombo vya muziki na kutoa unabii hekaluni.
  • Baadhi ya vyombo vya mziki vilivyokuwepo ni kinanda, kinubi, tarumbeta na matoazi.
  • Zaburi ya 50, 73-83 inasemekana zimetoka kwa Asafu. Na pia inawezekana baadhi ya zaburi hizi zimeandikwa na wanafamilia wake.