sw_tw/bible/names/abijah.md

616 B

Abiya

Ufafanuzi

Abiya lilikuwa jina la Mfalme wa Yuda aliyetawala tangu 915-913 BC. Alikuwa mtoto wa mfalme Rehoboamu. Walikuwepo watu wengine walioitwa Abiya katika agano la kale. Watoto wa Samweli Abiya na Yoeli walikuwa viongozi wa wana wa Israeli huko Belisheba. Kwa kuwa Abiya na kaka yake hawakuwa waaminifu watu walimuomba Samweli ateue mfalme mwingine wa kuwaongoza. Abiya mwingine ni yule aliyekuwa kwenye hekalu la kinabii wakati wa mfalme Daudi. Abiya lilikuwa jina la mtoto wa mfalme Yeroboamu. Abiya pia lilikuwa jina la kuhani mkuu aliyerudi na Zerubabeli Yerusalemu toka utumwani Babiloni.