sw_tw/bible/kt/lordssupper.md

775 B

chakula cha Bwana

Ufafanuzi

Msemo "Chakula cha Bwana" unatumika na mtume Paulo kumaanisha mlo wa Pasaka ambao Yesu alikula na wanafunzi wake usiku alipokamatwa na viongozi wa Kiyahudi.

Katika mlo huu, Yesu aliuvunja mkate wa Pasaka katika vipande na kuuita mwili wake ambao punde utapigwa na kuuliwa pia. Aliita kikombe cha divai damu yake, ambayo itamwagwa hapo punde atakapokufa kama sadaka ya dhambi. Yesu aliamuru kila mara wafuasi wake wanapokula mlo huu pamoja, wanapaswa kukumbuka kifo chake na ufufuo. Katika barua yake kwa Wakorintho, mtume Paulo aliendeleza kuimarisha zaidi chakula cha Bwana kama zoezi la mara kwa mara la waumini wa Yesu. Makanisa siku hizi husema "ushirika" kumaanisha chakula cha Bwana. Usemi "Meza ya Bwana" hutumika wakati mwingine.