sw_tw/bible/kt/lawofmoses.md

713 B

sheria, sheria ya Musa, sheria ya Mungu, sheria ya Yahwe

Ufafanuzi

Misemo hii yote inamaanisha amri na maelekezo ambayo Mungu alimpa Musa kwa ajili ya Waisraeli kutii. Misemo "sheria" na "sheria ya Mungu" zinatumika pia kwa ujumla kumaanisha kila kitu Mungu anachotaka watu wake kutii.

Kulingana na mazingira, "sheria" inaweza kumaanisha: Amri kumi ambazo Mungu aliandika katika jiwe kwa ajili ya Waisraeli. sheria zote alizopewa Musa vitabu vitano vya kwanza vya Agano la Kale. Agano lote la Kale (pia inajulikana kama "maandiko" katika Agano Jipya). maelekezo yote ya Mungu na mapenzi yake. Usemi "sheria na manabii" inatumika katika Agano Jipya kumaanisha maandiko ya Kihebrania (au "Agano la Kale").