sw_tw/bible/kt/kingdomofgod.md

722 B

ufalme wa Mungu, ufalme wa mbinguni

Ufafanuzi

Usemi wa "ufalme wa Mungu" na "ufalme wa mbinguni" zote zinamaanisha utawala wa Mungu na madaraka yake juu ya watu wake na viumbe vyote.

Wayahudi mara nyingi hutumia neno "mbingu" kumaanisha Mungu, ili kuepuka kutaja jina lake moja kwa moja. Katika kitabu cha Agano Jipya alichoandika Mathayo, aliuita ufalme wa Mungu kama "ufalme wa mbinguni," inawezekana kwa sababu alikuwa akiwaandikia zaidi Wayahudi. Ufalme wa Mungu unamaanisha Mungu kuwatawala watu kiroho pamoja na kuwatawala katika dunia ya kimwili. Manabii wa Agano la Kale walisema kuwa Mungu atamtuma Masihi kutawala kwa haki. Yesu, mwana wa Mungu, ndiye Masihi atakaye tawala juu ya watu wa Mungu milele.