sw_tw/bible/kt/justice.md

656 B

haki, adilifu

Ufafanuzi

Maneno haya yanamaanisha kuwatendea watu vyema kulingana na sheria za Mungu. Sheria za binadamu zinazo onesha kiwango cha Mungu cha tabia sawa kwa watu wengine.

Kuwa wa "haki" ni kutenda ya haki na mema kwa mtu mwingine. Pia inaashiria uaminifu na msimamo kufanya kilicho adilifu machoni pa Mungu. Kutenda kwa "haki" inamaanisha kuwatendea watu kwa njia iliyo sawa, nzuri na ya kufaa kulingana na sheria za Mungu. Kupokea "haki" inamaanisha kutendewa vyema chini ya sheria, aidha kulindwa kwa sheria au kuadhibiwa kwa kuvunja sheria. Wakati mwingine neno "haki" lina maana pana ya "utakatifu"au "kufuata sheria za Mungu."